Monday, July 9, 2012

Je ikitokea bongo hii si tutapaogopa hata bungeni?


Baada ya kuzidiwa na maswali kwenye kipindi cha televisheni LIVE, mbunge wa bunge la Jordan kwanza alivua kiatu na kumtandika mpinzani wake kabla ya kutoa bastola yake na kutishia kumpiga risasi jamaa aliyekuwa akimbana sana kwa maswali. Mbunge wa bunge la nchini Jordan alishindwa
 kuvumilia maswali ya mpinzani wake na
 kuamua kutoa bunduki kwenye kipindi
 cha televisheni kilichokuwa kikirushwa LIVE
 na televisheni ya Jordan.

Mbunge huyo aliyetajwa kwa jina la 

Mohammed Shawabka alikuwa kwenye
 kipindi cha mjadala wa mambo ya
 kisiasa kilichokuwa kikirushwa 
LIVE na televisheni ya Jordan.

Mjadala huo ulipamba moto pale mbunge 

huyo alipotupiwa maneno na mwanaharakati 
 wa masuala ya kisiasa, Mansour 
Sayf al-Din Murad akituhumiwa kuchakachua
 uchumi wa Jordan huku mbunge huyo pia
 akimtuhumu mwanaharakati huyo
 kuwa ni jasusi wa Israel.

Mbunge huyo baada ya kuzidiwa na maswali 

ya mwanaharakati huyo alianza 
kumrushia maneno makali.

No comments:

Post a Comment