Wednesday, July 18, 2012

MUNGU AKUPE MOYO WA SUBRA BI. Mwantum Mbilikira

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE,
INNALILLAH LA INNALLILAHI LAAJUN.
Tunawapa pole wale wote walioguswa na msiba wa mtoto wa Staff mwenzetu bi. Mwantum Rashid Mbilikira, ilikuwa ni siku ya majonzi kwa wote waliohudhuria msiba ambapo majira ya saa moja usiku siku ya jumatatu tarehe 16 Julai 2012 kilitokea kifo hicho cha malaika mdogo huyo ambaye hatutaacha kumkumbuka kwa makeke yake, raha zake na pia ucheshi wake na hasa hata kama mzazi amerudi na stress yaani msongo, malaika huyo kwa uwezo wake alikuwa anazitoa kwa namna ya kipekee na wazazi wake wamekiri na ni mashahidi wa jambo hili, chou chote cha TANZANIA E. COLLEGE kinaungana na familia nzima kuanzia hatua ya kwanza hadi ya mwisho katika wakati mgumu huu na wa majonzi kwa staff mwenzetu, tunaomba mwenyezi mungu ampe roho ya subra na ambariki liweze kumpita hili jambo mawazoni mwake maana hawezi kushindana na kudra pia matakwa ya mwenyezi mungu, mungu ndiye mtoaji na sisi tuko nyuma yake, mwenyezi mungu ambariki ustaadh Rashid pia naye ampe subra kama kwa mkewe vivyo hivyo, tunazidi kuwaombea na tunakumiss ofisini madam Mwantum, 
tu pamoja nawe!!
STAFF, TANZANIA E. COLLEGE.

No comments:

Post a Comment